Chris Brown ameendelea kuudhihirishia
ulimwengu mapenzi ya dhati aliyonayo kwa
mwanaye wa kike Royalty mwenye umri wa
mwaka mmoja. Baada ya kuamua album yake mpya kuipa jina la
mwanaye huyo ‘Royalty’, sasa staa huyo wa R&B
 ametoa cover ya album hiyo yenye picha ya yeye
 akiwa amembeba mtoto wake anaye onekana
amesinzia.

Toka Breezy afahamu kuwa ana mtoto na
aliyewahi kuwa model Nia Guzman, amekuwa
akionesha jinsi gani anajivunia kuwa baba na kwa
 kiasi gani mtoto huyo amemuongezea furaha
kwenye maisha yake.

Album ya ‘Royalty’ imepangwa kutoka Nov.27.
Share To:

Red Chapter

Post A Comment:

0 comments so far,add yours